Posts

Wimbo wa Dominika - Dominika 6 ya Mwaka C

Image

Sikiliza / Download Tafakari ya Dominika - Dominika 6 ya Mwaka C

Image

Maisha ya Mtakatifu Filomena wa Roma, FEBRUARI 17, 2019

Image
Filomena wa Roma ( 10 Januari 291 - 10 Agosti 304 ) alikuwa bikira wa ukoo tawala wa Corfu ( Ugiriki ) ambaye alianza kuheshimika kama mtakatifu mfiadini baada ya masalia kupatikana mnamo Mei 1802 katika Mahandaki ya Priscilla , Roma , Italia . Paliandikwa Pax Tecum Filumena (yaani "Amani kwako, Filomena"). Kabla ya hapo hakujulikana, lakini baadaye heshima ya Wakatoliki na Waorthodoksi wengi kwake imestawi sana hadi leo sehemu nyingi za dunia ikisaidiwa na njozi na miujiza iliyotokea kwa kuomba sala zake. Kati ya miaka 1837 na 1961 Kanisa Katoliki liliruhusu heshima hiyo katika liturujia pia. [1] Lakini wasiwasi wa wanahistoria umefanya jina lake liondolewe katika kalenda zote za watakatifu. 

MASOMO YA MISA, FEBRUARI 10, 2019

Image
MASOMO YA MISA, FEBRUARI 10, 2019 JUMAPILI, DOMINIKA YA  5 MWAKA C WA KANISA MWANZO: Zab. 95:6-7 Njoni, tuabudu, tusujudu, tupige magoti mbele za Bwana aliyetuumba; kwa maana ndiye Mungu wetu. SOMO 1 Isa. 6:1-2a, 3-8 Katika mwaka ule aliokufa mfalme Uzia nalimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana, na pindo za vazi lake zikalijaza hekalu. Juu yake walisimama maserafi; kila mmoja alikuwa na mabawa sita. Wakaitana kila mmoja na mwenzake, wakisema, Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, ni Bwana wa majeshi; dunia yote imejaa utukufu wake. Na misingi ya vizingiti yote imejaa utukufu wake. Na misingi ya vizingiti ikatikisika kwa sababu ya sauti yake aliyelia, nayo nyumba ikajaa moshi. Ndipo niliposema, Ole wangu! Kwa maana nimepotea; kwa sababu mimi ni mtu mwenye midomo michafu, nami ninakaa kati ya watu wenye midomo michafu; na macho yangu yamemwona Mfalme, Bwana wa majeshi. Kisha mmoja wa maserafi wale akaruka akanikaribia; nay...

TAFAKARI, FEB 10: VILIVYO VIDHAIFU KUPEWA THAMANI YA KUMTANGAZA MUNGU

Image
“MBEGU ZA UZIMA” Tafakari ya kila Jumapili Februari 10, 2019 DOMINIKA YA 5 YA MWAKA WA KANISA VILIVYO VIDHAIFU KUPEWA THAMANI YA KUMTANGAZA MUNGU Jumapili iliyopita tulisikia kuhusu wito wa Yeremia, na leo tuna habari tena ya wito wa Isaya na Petro. Mmoja anaweza kujiuliza kwanini Mungu anachangua watu kama hawa? Mungu anafikiria nini? Lakini ukweli ni kwamba hili sio jambo geni kwa Mungu. Abrahamu alichaguliwa na Mungu akiwa mzee ili awaweze kuwa Baba wa taifa la Israeli, Mungu alimchagua Musa ambaye alikuwa hawezi kuongea vizuri, kigugumizi ili kukabiliana na Farao na kuongoza wana wa Israeli, Kijana mdogo tena mchungaji, Daudi alichaguliwa na Mungu kuwa Mfalme wa Israeli. Na pia Sauli ambaye alikuwa mtesi wa Kanisa anachaguliwa na Yesu kuwa chombo chake kiteule cha kuhubiria Injili yake. Hii yadhihirisha kwamba Mungu anafanya kadiri ya mapenzi yake. Vyombo anavyo vichagua Mungu ni kutoka katika ulimwengu wetu, hata kama sisi tunaviona ni dhaifu. Tunaweza tukak...